Hivi karibuni nimeongea na mchungaji wangu ambaye amenishauri niendelea kumwomba Mungu na kufunga lakini hii hainisaidii kwasababu bado naendelea kutoka nje ya ndoa.
Najua natakiwa kuacha lakini sijui ni vipi. Tafadhali nisaidieni-
- Najua story yangu itawafanya watu wengi
wanifokee lakini nitashukuru kwa msaada wowote nitakaoupata. Niliolewa
na mume wangi April 2010. Ingawa kwa mara ya kwanza sikuwa na nampenda
mume wangu, lakini nilikuwa nazidi kuzeeka na sikuweza kumpata mwanaumbe
yeyote wa dini yangu na kabila langu, wazazi wangu walinitambulisha kwa
huyu mwanaume na kunilazimisha niolewe nae.
Mara ya kwanza natoka nje ya ndoa ilikuwa bahati mbaya. Nilikutana na mpenzi wangu wa zamani na tukabadilishana Pins zetu za BlackBerry. Huwa tunachat mara zote na nikaanza kutoifurahia ndoa yangu kwahiyo nikamshawishi huyu ex wangu. Tukaanza kukutana na kuanza kufanya mapenzi. Baadae akahamia kutoka huku mjini na kuhamia mji wa mbali na hatimae mahusiano yetu yakaishia hapo.
Kutoka hapo nimekuwa na mahusiano na wanaume wengine wane ikiwemo mume wa rafiki yangu. Nina watoto wawili na mume wangu lakini siridhiki katika mapenzi.
Mume wangu ni mpole na ananipenda, na nimetokea kumpenda lakini nashindwa kuacha mahusiano yangu ya nje ya ndoa. Kinachonisikitisha zaidi ni kwamba mume wangu hajui chochote kile kinachoendelea. Simpi nafasi yoyote ile ya kuwa na wasiwasi na mimi. Nafuta sms zote kwenye simu yangu ingawa huwa hana tabia ya kuchungulia kwenye simu zangu. Nahakikisha hagundui chochote kwasababu nataka familia yetu isisambaratike.
Hivi karibuni nimeongea na mchungaji wangu ambaye amenishauri niendelea kumwomba Mungu na kufunga lakini hii hainisaidii kwasababu bado naendelea kutoka nje ya ndoa.
Najua natakiwa kuacha lakini sijui ni vipi. Tafadhali nisaidieni
Recent Posts
WADAU HII NI HATARI KATIKA MAPENZI
Aina mpya ya vimelea vya ugonjwa wa kisonono au "gono" ambavyo vinahimili dawa(resistant to [...]
Mar 01, 2016SEHEMU YA PILI SIKU YA HARUSI YANGU NITAVAA GAUNI MOJA KATI YA HAYA..
SIKU YA HARUSI YANGU NITAVAA GAUNI MOJA KATI YA HAYA.. ACCESORIES[...]
Oct 12, 2014NANI ASIE JUA MAUMIVU YA MAPENZI? JE UTATOA UHAI WAKO KWA WANGAPI? NI SWALI LA KUJIULIZA; MWANAFUNZI CHUO CHA UHASIBU AJICHOMA KISU TUMBONI BAADA YA KUMFUMANIA MPENZI WAKE AKIWA NA KIMADA
Mwanafunzi aliefahamika kwa jina moja la Moza alie mwaka wa kwanza katika chuo cha Uhasibu T[...]
Oct 12, 2014ANGALIA PICHA SHINDANO LA MISS REDDS JANA
Pichani ni Washiriki waliochaguliwa kuingia kwenye hatua ya tano bora katika shinda[...]
Oct 12, 2014