0


Admin naomba post hii ...Mimi nimsichana wa miaka 25 sasa ..Nashindwa hata nianzie wapi ila kifupi mimi sina bahati na wanaume at all..Nina sura na umbo zuri na amini hilo kwani kila napokwenda lazima nitongozwa ama nisumbuliwe na wavulana njiani mpaka nimezoea...ila tatizo linakuja pale napomkubalia mwanaume na kuwa wapenzi ..wakishapata wanachohitaji hawakai kabisa...nimetembea na wavulana wengi tu kila anaenipata anakaa kidogo na kuanza visa na kuniacha ...Mie najua kupenda naamini....Marafiki zangu wanaolewa ila mimi hakuna hata aliye nivisha pete na uzuri wangu huu..hadi najilaumu labda umbo langu limekaa kistaree tu na sio wa kuolewa...kwa sasa nimekata tamaaa nawachukia wavulana kila atakaye nitongoza nahisi anataka kitu tu alafu akimbie...Nisaidieni kwa Ushauri...

Post a Comment

Kama umependezwa na hii stori toa maoni yako kama unayo

 
Top