0
http://wwwdelivery.superstock.com/WI/223/1433/PreviewComp/SuperStock_1433R-163019.jpgKila binadamu hupenda jambo fulani. Mapenzi ya mtu juu ya jambo yaweza kumvutia kiasi kwamba anaweza kupoteza welekeo wa maisha yake. Watu hupenda hadi kileleni. Hapa ndipo mtu aelewi hili wala lile. Hali hii si tu kwa vijana wanaoingia katika umri wa balehe bali hata kwa wale waliovuka umri huu. Kweli kila mtu anahaki ya kupenda. Na mapenzi haya yalianza pale binadamu walipoanza kuishi pamoja kama mke na mume kama vitabu vyetu vya dini vinavyoelekeza, ambavyo ni Biblia na Kuruhani.

Napenda kuwa muwazi sana juu ya aina ya penzi ninalozungumzia. Ni yale mahusiano ya kimwili yaliyopo kati mwanamke na mwanaume. Haya ndiyo mahusiano ninayozungumzia na sizungumzii yale ya watu wa jinsia moja. Mapenzi hayauzwi na ayachagui rangi wala kabila.Mapenzi ni kitu asilia ambacho  humkuta mtu juu ya mtu mwingine ambaye anaweza kuwa mwanamke kwa mwanaume au kinyume chake. Na hawa kila mmoja hutokea kumpenda mwenzake mpaka kufikia kilele cha penzi.


Angalia mfano huu; umepita wapi na kutembea mikoa mbalimbali au wilaya, tarafa, kata, vijiji na mitaa mingapi? Umekutana na wangapi wazuri (wanawake au wanaume), na ulimpenda yupi. Inawezekana kati ya uliowachagua hakuna hata mmoja kati ya wale uliokutana nao ukaridhia kuwa naye. Lakini ulikutana na kijana mmoja ambaye amekuvutia sana zaidi ya asana na mahusiano ukaanza kuanzisha mpaka leo ni mke wako au mchumba wako. Hapo ndipo ninaposema “love is something natural” na si kitu cha kubahatisha tu.

Na ieleweke kwamba mke mzuri ni wako tu, na mme mzuri ni wako tu. Hakuna ubishi kwa hili. Na pale unapoona kuwa mke au mme wako si mzuri basi ulikosea wakati wa uchaguzi  wako. Hapo huna budi kuonyesha unampenda kama kitabu hiki kinavyoeleza uk.6 & 7. Na ujue kwamba kila mtu ana haki ya kupendwa na mme, mke au mchumba wake. Penye upendo pana mapenzi ya kweli.


Kazi hii imeandaliwa na


CHIWAMBO, A. R. (2011) 

BA SOCIOLOGY

TEOFILO KISANJI UNIVERSITY (TEKU).

Post a Comment

Kama umependezwa na hii stori toa maoni yako kama unayo

 
Top