0

Katika ulimwengu wa mapenzi hakuna Jambo linaumiza Roho na Moyo kama kuachana na Mpenzi wako ambae ulimpenda kwa dhati na kuhisi  ndie aliestaili kuwa chaguo lako katika maisha ya hapa Duniani.

Suala la kuachana  limeumiza  watu wengi wanaume kwa wanawake vijana kwa watu wazima na hili hutokea tu kwa wale watu ambao hawakujiandaa kuachana au kupokea taarifa ya kuachana au kutengana,kwa mujibu wa tafiti mbali mbali zilizofanywa zinaonesha sailimia kubwa ya wanawake huumia zaidi pindi wanapoachwa kuliko wanaume,nah ii inatokana na ukweli kwamba wanaume wanakuwa wameshaa tayarisha mazingira baada ya kuachana.

Kila mmoja anatambua kuachana si jambo jema katika maisha ya  mahusiano lakini kuna wakati hunabudi kufanya maamuzi haya mazito kutokana na ukweli kwamba unakuwa umechoshwa na tabia,mwenendo au hata maisha ya huyo mpenzi wako labda amekuwa mwongo sana,msaliti mnoo,msherati na tabia nyingine nyingi zisizo stairi na kuweza kukuletea matatizo katika maisha ya kila siku ya hapa Duniani.

Leo Mpita Njia nakuletea njia chache kati ya nyingi ya kuweza kuachana na mpenzi wako pasipo kuumia Roho kama ifuatavyo.
 
1.JIULIZE KWANINI UNATAKA KUACHANA NAE
Ukijiuliza kwanini unataka kufanya maamuzi hayo mazito utagundua ukweli uliojificha ndani yake kama kweli upo sahihi kwa maamuzi hayo au unasukumwa na Hasira kufanya maamuzi hayo,ukigundua si hasira jiulize kwanini imekuwa sasa na haikuwa siku za nyuma ya mahusiano yenu?hapa ndipo utapopata utofauti ambao utakupa kujiamini kwa maamuzi utayofanya,na kama utaona unakila sababu ya kuachana nae kutokana na utofauti wenu amini kabsaa hauta umia moyo kwa maamuzi yako.

2.ANDIKA SABABU ZA WEWE KUACHANA NAE
Ndioooo unapaswa kuandika sababu za wewe kuamua kufanya maamuzi hayo ya kuachana nae kwani usipotambua sababu itakurahisi kwako kuhisi maamuzi yako si sahihi lakini ukiandika utaona haja na kusimamia katika uamuzi wako,

mfano pengine amekusaliti mara tatu,amekudanganya sanaa,ametembea na rafiki yako,unatumia muda mwingi kumfikili yeye,unatumia ghalama kubwa sana kuwa nae,hadhamini upendo wako,hana mapenzi ya dhati kwako,amekutangazia mbovu kwa rafiki zako,umekuta sms za wa watoto wa kike ktk simu yake ,unaogopa kupewa magonjwa,hupendi kushare mapenzi nk.

ukiandika list ya vitu hivi hakika hutaona sababu yaw ewe kuendelea kuwa na huyo mtu kwani utajionea huruma kwa mambo mengi kiafya,kiuchumi na hata kisaikolojia.hivyo ukifanya maamuzi hutaludi nyuma wala kuumia moyo.

3.WAAMBIE RAFIKI ZAKO WA KARIBU
Siku zote Rafiki wana nafasi kubwa sana ya kukusaidia kuepukana na mambo ya hatari ila kama hao rafiki ni wazuri ,ikitokea unataka kufanya maamuzi ya kuachana na mpenzi wako unaweza kuwashirikisha wale rafiki ambao ni msaada kwako.

maana wao watatambua kuwa umeachana na boy wako hawawezi kukuuliza afya ya mtu wako,au kukukumbusha mambo ambayo wanajua yatakuumiza roho na kukukosesha amani kama utayakumbuka hivyo utakuwa umewafunga wasiweze kukukumbusha, lakini pia rafiki hao ndio watakao kuweka busy kwa kukupigisha stori,
kuchat na kumsahau Yule aliekupa shida kwa muda mrefu,hivyo kabla yaw ewe kumwambia mpenzi wako kuwa wewe nay eye bhasi hakikisha unawatu au kuna vitu vya kukufanya uwe busy hivyo nafasi yake katika akili yako itakuwa ndogo sanaa.

4.MWAMBIE AJUE MMEACHANA
Jambo lamsingi sana katika kufanya maamuzi ya msingi pia ni kuwa wazi kwa kila jambo hivyo baada ya kuandaa mazingira teyari usiishie kukaa kmyaa bali unapaswa kumwambia ukweli kuwa mimi na wewe kuanzia sasa BHASSSSSS TENA,

kwakufanya hivi utakuwa umejiweka mahali pazuri kwani hata kutafuta kwa kujuwa yupo huru kuendelea na mambo yake,angalizo hapa wengi wakishaambiwa hivi huwa wanakuwa wagumu kuelewa lakini wewe simamia hoja zako kusema Enough,ikipita wakati atapokea hali ile na kuendelea na maisha yake na wewe kuendelea na maisha yako ya kila siku pasipo kupata bhughuza kutoka kwake na kufanikiwa lengo lako.

5.JIPANGIE SIKU NA  TAREHE YA WEWE KUFANYA MAAMUZI HAYO.
Jambo la mwisho lazima ujipangie siku na tarehe ya  wewe kufanya maamuzi hayo hii itakufanya upate nafasi ya kuweza kumtoa huyo mtu katika akili yako,mawazo yako na hata moyo wako taratibu taratibu mpaka siku unafanya maamuzi ya mwisho moyo wako hautashtuka kwa kuwa umeshajiandaa na hilo jambo na hautaweza kujutia maamuzi yako hata siku moja kwa kuwa ulikuwa na kila sababu ya kuachana nae . 

Nimalizie kwa kusema kwamba katika kufanya maamuzi ya kuacha na mtu lazima uangalie vitu vingi vinavyowazunguka na kukusukuma kufanya hivyo ili wewe uwe kati,ka hali nzuri japo si vizuri kufanya maamuzi hayo wakati ukitawaliwa na hasira kwani hapo utakuwa unaongozwa na hasila na si uhalisia.

Post a Comment

Kama umependezwa na hii stori toa maoni yako kama unayo

 
Top