0
Leo nilikuwa nasoma research iliyofanywa na Dr(PhD) Brown ambaye pia ameandika kitabu kinaitwa "Gifts of imprefection" anyways, huyu Dr. alikuwa amekaribishwa kwenye kipindi cha Oprah katika OWN kuongelea kwa nini watu wengine wanakuwa na furaha ya maisha/kuishi na wengine wanakuwa wanyonge mara zote.
Mara nyingi watu wanakwambia "ningekuwa na pesa nyingi, matatizo yangu yote yangeisha na hata nisingelalamika kuhusu maisha, ningekuwa mwenye furaha saa zote." Well, kama tunavyoona katika dunia hii, hata wenye pesa sana wanamatatizo tena labda kupita kiasi in a sense kwamba hawakai kwa amani na mengine mengi. Ila tusisahau wapo pia wenye hela zao na wanakaa tuu kwa amani pia ila ni wachache. 

Anyways, matokeo kutoka utafiti wa huyu Dr. ulimwonyesha kwamba; Watu wengi walioonyesha kufanikiwa katika maisha yao mfano ya kindoa/kimapenzi/kiurafiki, walionyesha kuwa wakiishi maisha yako "dedicated to the cause" yaani sio mguu mmoja ndani mmoja nje. Pia matokeo yalionyesha kwamba, watu kama hawa, wanawake haswa (Ila wapo hata wanaume ambao wakishaamua kujidedicated katika relationship zao ni wanafanya kweli), anyway, huyu Dr. alisema kwamba, watu wengi wanaofanikiwa katika maisha yao ya ndoa, na nikisema kufanikiwa namaanisha wanaishi kwa amani, upendo, na furaha na wenza wao ni kwasababu watu kama hao wameweza kujikubali (accepting themselves) na kukubali kwamba they are WORTH OF LOVE AND BELONGING. Huyu Dr. alingundua kwamba yaani watu ambao wameshajiaccept na kujua kwamba they can love and belong, it didn't matter what circumstance ya maisha waliyokuwa nayo wedha ni nzuri ama mbaya, watu wenye karactaristics za aina hii wanaweza kuishi maisha ya furaha sana. 
kuelezea kwa kifupi ni kwamba; mara nyingi watu tunaonaga kwamba, ndio tunajipenda na tuko worthy kupendwa na kuwapenda wengine lakini tunasikia kijipenda zaidi kama labda tungeongezwa cheo kazini ama labda kama tungepata gari zuri zaidi na tulilokuwa nalo kwa sasa, ama kama tungeongeza elimu lbada tungejipenda zaidi. Yaani a lot of times watu wanakuwa unhappy kwasababu binadamu ni mgumu kuridhika na alichonacho. Mara nyingi pia mambo yakutoridhika hutokana pia na kupenda kuonekana na watu kwamba wewe ndo uko juu ama mbele zaidi ya wengine ama kupenda kupewa sifa kila mara.
Mara nyingi unakuta watu kama hawa hawanafuraha moyoni ya kila mara kwamaana wanarely on whats next I can do so people can see me again and praise me.

Watu ambao wanaweza kugundua walipokosea na kujikosoa wenyewe au kutokasirishwa wanapo kosolewa ni wachache of course lakini kwa mujibu wa huyu Dr. alichoweza kujifunza ni kwamba watu kama hawa ndo ambao waliweza kuonyesha kuishi maisha ya furaha zaidi. Yaani imani zao kuhusu maisha zimeweza kuwa ndo mwanga wa kila wanachokifanya kila siku wedha kitu wanachokifanya kinakuwa na mafanikio ama hapana bado wanaridhika na siku yao na kukubali kwamba kuna kesho I can do better. Watu kama hawa, hawajifichi wanapochapia ama mambo yanapokwenda ovyo ama wanapo aibishwa, wameshajifunza jinsi ya kudeal na matatizo kiasi cha kwamba wanajua jinsi ya kuface na huhandle most life's challenges na kuibuka imara.
Hivyobasi, hata sisi ambao bado we are working on kuridhika na maisha/becoming/being content with maisha there are a few things we can do ili kuweza kufikia stage kama hizi za walioridhika na wenye furaha katika moyo na maisha kiujumla.
  • Pointi ya kwanza ni kulet go of exhaustion - katika mihangaiko yako ya siku nzima make sure unaweka muda wa kupumzika. Kwa mfano; mara ngapi unajikuta umehangaikaa the whole day na huoni ulichokifanya lakini kama ungeupa mwili na akili nafasi ya kupumzika ungeweza kuisaidia akili kuwa na uwezo wa kufikiria vizuri na juu tena zaidi. Hivyo according to "Whole Hearted People advise" wanasema kwamba ili kuwa na mafanikio na kuweza kufikia kima cha kuwa content/kuridhika na maisha na kuweza kuwa na furaha; KNOW WHEN TO STOP AND REST!
  • Tafuta muda wa kufanya kitu unacho enjoy. Rudi na kuangalia ninini kipaji chako na jaribu kukiendeleza. Mfano; kushona, kufuma, kusoma vitabu, kuimba, gardening etc. sio lazima ufanye siku nzima lakini jipe muda wa kuweza kufanya vitu unavyo enjoy which a lot of times vinakuwa ni vipaji. Na hata wakati mwingine kuwa creative anzisha kitu chako mwenyewe.
  • Kuiacha roho/moyo/akili iwe tulivu (staying calm). Mara nyingi kama binadamu si rahisi kujiambia calm down and get a prompt response, hivyo basi ni muhimu kuchukua muda na kujituliza akili. Kuwa mrahisi wa kusikiliza na kujisikiliza zaidi badala ya kuongea wakati wote. Wanasema mara nyingi mtu ukiweza kustay calm, you can be able to hear what your mind and body is trying to tell you. Ila kwasababu we are so busy telling ourselves what to do all the time basi we shut down what really needs to speaks to us which is our soul.
  • Make room kucheza na familia yako, watoto wako, mume wako n.k. Huu ndo ule wakati wa kuangalia family shows together, kucheza board games (i.e. snake and ladder lol), karata ama hata kupiga hadithi ama kuangalia picha za zamani/utotoni na harusi and laugh, sali ama soma neno la Mungu pamoja na familia etc.

Kitu nilichogundua wakati nasoma na kumsikiliza huyu Dr. ni kwamba, sisi wataswahili tunapendaga kuwa serious sana na maisha and thats why saa nyingine yanatufrustrate. Wakati mwingine we need to let it loose and enjoy just simple things in life, i.e. kukaa na watoto wetu na kuchora funny pictures ama kufanya vitu tuu ambavyo vitakufanya ujione hauko katika element yako lakini at the same time you are enjoying doing it kwasababu you are feeling happy and good. Kumbuka LIFE IS TOO SHORT TO BE STRESSED OUT ALL THE TIME. ITS JUST NOT WORTH IT!!!


Post a Comment

Kama umependezwa na hii stori toa maoni yako kama unayo

 
Top