0




Habari Admin,
Naombeni msaada wa maawazo yenu, nimegundua kuna mwanamke anatembea na mume wangu, mume wangu alikataaaaaa kwa mara ya kwanza, lakini baada ya kufatilllia na kuchunguza kwa muda mrefu nikaja kuhakikisha ni kweli kabisa, mwanamke anaomba msamaha kwamba wataachana na hatorudia tenaa, na mume wangu pia anasema hatorudiaa,

Nimeumia sana mwenzenu, nimeumia kupita kias, kwakuwa nilimpenda, nilimheshimu, nilimjali sana mume wangu, nilikuwa teyari kumuachia yeye kila kilicho changu, nilimsikiliza sana, sikutegemea kama atakuja kunitenda hivi, imekia kipindi najuta kwanini niliolewa nay eye,  sikutegemea kabisa kutokana na muonekano alio nao,,, details zoote za huyo mwanamke wake niko nazo, niliomba niprintiwe kupitia mitandao ya simu wanayotumia, niko nazo mkononi, staki kuamini, ninalia kama mtoto mdogo, ni bora niibiwe pesa nitatafuta, kuliko kuibiwa penzi,, nitalipata wapi,,
Nimechanganyikiwa, nataka kuondoka kwenda kwetu nikapumzike, nimwache kwanza, maana kila nikimuona Napata hasira natamani kumkaba kabisa, nimemchukia mno,,, sina amani ya kuwa nay eye, hali hii hadi lini?? Nifanyaje?

Post a Comment

Kama umependezwa na hii stori toa maoni yako kama unayo

 
Top